Chuo Kikuu cha Tsinghua cha China kimechaguliwa na kuchukua nafasi ya kwanza katika vyuo vikuu vizuri zaidi barani Asia mwaka 2019 na kuwa chuo kikuu cha kwanza cha China kufikia nafasi hiyo.
Chuo kikuu hicho kimechukua nafasi ya chuo kikuu cha taifa cha Singapore ambacho kilichukua nafasi ya kwanza tangu mwaka 2016 kutokana na ongezeko kubwa katika mazingria ya kufundisha, athari za dondoo na mtazamo wa kimataifa.
Aidha, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Hong Kong, China kimechukua nafasi ya tatu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |