Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Jamie Mcgoldrick amesema jumla ya dola za kimarekani milioni 20 zinahitajika katika Ukanda wa Gaza ili kuwasaidia watu 1,700 waliojeruhiwa vibaya katika maandamano yaliyoanza mwaka mmoja uliopita dhidi ya Israel. Amesema huduma za matibabu huko Gaza ni mbaya, na ombi hilo la kuchangiwa fedha za dharura pia linalenga kuimarisha mfumo wa afya kwa njia ambayo kwa sasa haijaungwa mkono.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |