• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wabunge waongezewe mishahara, Wakenya wamewageuza benki – Atwoli

    (GMT+08:00) 2019-05-09 20:28:38

    Siku chache baada ya juhudi zake za kutaka serikali iwape wafanyakazi nyongeza ya mishahara ya asilimia 15 kugonga mwamba, Katibu Mkuu wa COTU Francis Atwoli sasa anaunga mkono nyongeza ya mishahara ya wabunge.

    Atwoli amesema mishahara ya wabunge inapasa kuongezwa ili kuwawezesha kutosheleza matakwa ya wananchi ambao huwaomba pesa kila mara.

    Atwoli amesema tabia ya Wakenya ya kuwaomba wabunge pesa kila mara ndiyo imechochea ufisadi nchini Kenya. Ameongeza kuwa wabunge wengi wanalazimika kutoa fedha nyingi kwa wananchi wakati wanapopata matatizo kama vile misiba na hata magonjwa. Kinara huyo wa COTU alisema kuna baadhi ya wabunge ambao hutumia kati ya Sh300,000 na Sh600,000 kila wiki wanapotembelea maeneobunge yao; pesa ambazo wanatarajiwa kutoa kutoka kwa mishahara yao. Kiongozi huyo wa Cotu alitoa wito kwa Wakenya kushiriki katika shughuli za kuwaletea mapato kama vile kilimo badala ya kutegemea viongozi wao kwa mahitaji yao ya kila siku. Kauli hiyo inajiri baada ya wabunge na maseneta kujitengea shilingi bilioni 936 kama marupurupu ya nyumba iliyopendekezwa na Tume ya Huduma za Bunge (PSC) 2018.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako