kipa Kepa Arrizabalaga na mshambuliaji Edin Hazard wa Chelsea wameiwezesha timu yao kutinga fainali kwa ushindi wa penalti 4-3 kufuatia sare ya jumla ya magoli 2-2 ndani ya dakika 210 kwenye mechi mbili za nyumbani na ugenini.
Nao washika bunduki wa jijini la London Arsenal, wao walikuwa ugenini uwanja wa Mestalla walipovaana na Valencia. Mshambuliaji wa kimataifa wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang alipiga hat trick kwa mabao yake dakika ya 11, 69 na 88 ikiwalaza wenyeji Valencia kwa bao 4-2.
Goli la Valencia lilifungwa na Kevin Gamiero dakika ya 11 na 58. Kwa matokeo hayo, Arsenal inakwenda fainali kwa ushindi wa jumla ya magoli 7-3. Hivyo Arsenal itakutana na Chelsea katika mchezo wa fainali hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |