Mshambuliaji wa timu ya Golden State Warriors ya nchini Marekani inayoshiriki ligi kuu ya kikapu nchini humo (NBA) Kevin Durant atakaa benchi na kukosa mechi ya 6 itakayochezwa usiku wa leo mjini Houston Marekani kutokana na kuumia wakati timu yake ilipocheza mechi ya 5 na Houston Rockets Jumatano hayo yamebainshwa na kocha wa timu hiyo Steve Kerr.
Durant huenda akarejea uwanjani katika mchezo wa 7 wakati timu yake itakapocheza Jumapili katika uwanja wa Oracle.