Waziri wa mambo ya nje wa Palestina Riyad al-Maliki amesema mpango wa amani ya Mashariki ya Kati utakaotolewa hivi karibuni na Marekani haulengi kuhimiza amani, bali kutoa masharti ya kujisalimisha. Amesema nchi yake haikatai juhudi zozote za amani, lakini kwa bahati mbaya juhudi zinazofanywa na Marekani sio za amani. Ameongeza kuwa baada ya Marekani kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel, maamuzi yaliyofanywa na serikali ya Marekani yote yameonyesha kuwa haizingatii maisha na haki za watu wa Palestina wala makubaliano na sheria ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |