Harambee Stars inarejea katika michuano hii baada ya kuikosa mara kadhaa, itaondoka Mei 31 kwenda Ufaransa kuweka kambi ya kujifua, wakiwa jijini Paris, watamenyana na Madagascar Juni 7 na Gambia Juni 15 michezo ya kirafiki.
Katika michuano hiyo ya AFCON, Kenya ambayo inajivunia mchezaji wake Victor Wanyama anayekipiga klabu ya Tottenham Hotspur ya Uingereza itakutana na Algeria Juni 23, kasha itavaana na wenyeweji wao Tanzania Juni 27 kabla ya kukutana na Senegal Julai 1.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |