Katika hotuba aliyotoa Xi Jiping kwenye Mkutano wa mazungumzo ya ustaarabu wa Asia unaofanyika leo hapa Beijing, amezitaka nchi mbalimbali ziwe na usawa na kuheshimiana, kutupilia mballi kiburi na maoni ya upande mmoja katika kuingiliana na kufundishana ustaarabu wa aina mbalimbali, ili kuongeza uelewa kuhusu tofauti kati ya ustaarabu wa aina mbalimbali.
Rais Xi amesema, kila aina ya ustaarabu ina thamani ya uwepo wake. Kuna rangi na lugha tofauti tu kati ya binadamu, ustaarabu wa binadamu una aina mbalimabli za rangi tofauti, hata hivyo, hakuna tofauti kati ya uzuri na ubaya au kati ya juu na chini; kama binadamu wa rangi fulani wanajivuna na kuona ustaarabu wao ni bora zaidi kuliko wengine, na wanajaribu kujenga upya ustaarabu mwingine hata badala yake, uelewa huu ni wa kijinga, na utaleta balaa. Amesema, China inapenda kushirikiana na nchi mbalimbali katika shughuli za kulinda mali ya urithi wa utamaduni wa Asia, ili kutoa uhimili wa lazima kwa kurithi vizuri ustaarabu wa binadamu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |