• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Serikali kutoa kipaumbele sekta ya kibinafsi

    (GMT+08:00) 2019-05-15 17:22:43
    Wizara ya Viwanda na Biashara imesema mwelekeo na vipaumbele vya bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/20 ni pamoja na kuifanya sekta binafsi kuwa injini ya uchumi. Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda, alipokuwa akisoma hotuba ya bajeti yake bungeni ambapo bunge limuidhinishie Sh bilioni 100.38, kiasi ambacho ni pungufu la Sh bilioni 48.88 ikilinganishwa na bajeti inayoisha.

    Kakunda alisema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi ili kuhakikisha wadau wote wanatoa mchango unaohitajika katika ujenzi wa uchumi wa Taifa. Alisema pamoja na mazingira rafiki ya uwekezaji katika viwanda na biashara, utekelezaji wa mpango wa kuboresha mazingira ya biashara (blue print) unaangaliwa kuwa sehemu ya tiba ya changamoto ambazo zinaitatiza sekta binafsi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako