Mcheza tenisi bora duniani Maria Sharapova ameondolewa kwenye mashindano ya wazi ya tenisi ya Ufaransa kutokana na kuumia bega.
Mchezaji huyo raia wa Russia ametangaza kuwa hatashiriki michuano hiyo ya tenisi mwaka huu ambayo yanatarajiwa kuanza Mei 26. Sharapova hajaonekana uwanjani tangu mechi yake ya mwisho dhidi ya Daria Kasatkina mwezi Januari mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |