Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza mpango wa mageuzi ya mfumo wa uhamiaji wa nchi hiyo, yanayolenga kuwapendelea wahamiaji wenye ujuzi wa hali ya juu na kuzuia uhamiaji unaotokana na uhusiano wa kifamilia. Akizungumza kwenye Ikulu ya Marekani, rais Trump amesema anataka kuanzisha mfumo wa uhamiaji wenye haki, wa kisasa na kufuata sheria nchini Marekani. Pia amesema mabadiliko makubwa wanayofanya ni kuongeza idadi ya wahamiaji wenye ujuzi wa hali ya juu kutoka asilimia 12 hadi 57 ili kuifanya Marekani iwe na nguvu kubwa ya ushindani duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |