Msemaji wa Kamandi ya operesheni za pamoja ya Iraq Yahya Rasoul amesema roketi aina ya Katyusha ilirushwa dhidi ya eneo la wazi karibu na ubalozi wa Marekani, katikati mwa Baghdad, Iraq, lakini haikusababisha vifo ama majeruhi yoyote. Kwa mujibu wa ofisa mwingine wa usalama ambaye hakutaka jina lake kutajwa, vikosi vya usalama vimegundua kifaa cha kurushia roketi katika eneo la Baladiyat, mashariki mwa mji huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |