Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekataa ombi la Russia la kujadili utungaji wa sheria ya lugha ya Ukraine. Wajumbe 5 kati ya 15 wa Baraza hilo walipiga kura kuunga mkono ombi hilo, idadi ambayo haikufikia kigezo kinachohitajika cha kura 9 kupitisha ajenda ya muda yenye utata ya Baraza la Usalama. Kabla ya kura hiyo, balozi wa Russia kwenye Umoja wa Mataifa Vassily Nebenzia alisema sheria mpya ya Ukraine ilikiuka Makubaliano ya Minsk yaliyopitishwa na Baraza la Usalama. China imeeleza kusikitishwa na hatua ya Baraza la Usalama kukataa ombi la Russia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |