Mkuu wa majadiliano ya Brexit ya Umoja wa Ulaya Michel Barnier amesema Umoja huo unajiandaa na hali mbaya zaidi ya Brexit, yaani Uingereza kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya bila ya makubaliano yoyote. Barnier amesema Umoja huo umetoa machaguo yote kwa Uingereza kutoka Soko la pamoja hadi Umoja wa Forodha ama Makubaliano ya Biashara Huria, na sasa unasubiri jibu wazi kutoka Uingereza. Bunge la Uingereza lenye mpasuko liko tayari kupiga kura kuhusu muswada mpya wa sheria kuhusu Brexit.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |