• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Sevilla yatua bongo, Tarimba awapa neno.

    (GMT+08:00) 2019-05-22 08:17:59

    Klabu ya Sevilla ya Uhispania ambao wamewahi kuwa mabingwa wa ligi ya Ulaya wamewasili jana nchini Tanzania jijini Dar es Salaam tayari kwa mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya mabingwa wa nchi hiyo Simba.

    Msafara wa wachezaji 18 pamoja na viongozi wametua tayari kwa kipute kitakachopigwa kesho uwanja wa Taifa jijini humo, mkurugenzi wa utawala na udhibiti wa kampuni ya SportPesa Tarimba Abbas amesema ujio huo wa Sevilla umeanza kuitangaza Tanzania katika ramani ya dunia hususani upande wa soka na utalii, huku akiwaonya Sevilla kutoichukulia Simba poa katika mechi yao hapo kesho.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako