Rais John Magufuli wa Tanzania amewaamuru maofisa wote wa ngazi ya juu wa serikali kutumia huduma za simu zinazotolewa na kampuni ya simu inayomilikiwa na serikali, TTCL.
Akizungumza katika hafla iliyotangazwa moja kwa moja na Televisheni ya Taifa nchini humo TBC, rais Magufuli amewapa maofisa hao siku 30 kuanzia jana kuanza kutumia huduma za simu za TTCL, na kuongeza kuwa kufanya hivyo kutaongeza kipato cha kampuni hiyo.
Tanzania ina kampuni binafsi kadhaa zinazotoa huduma za simu ikiwemo Airtel, Vodacom, Halotel na Tigo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |