Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha kwa kauli moja azimio la kuongeza muda wa Tume ya Msaada ya Umoja huo nchini Iraq UNAMI hadi Mei, 31, mwakani. Baraza hilo lenye wajumbe 15 limetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuendelea kutoa msaada kwa Iraq ili kuunga mkono juhudi zake za kibinadamu, kuleta utulivu, kufanya ujenzi mpya na maendeleo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |