Fidia hiyo inahusiana na uharibifu wa mali na kupoteza kwa mapato katika jumba lote la 14 Riverside, ikiwemo hoteli ya DusitD2 Hotel.
Wamiliki wa jumba hilo walikuwa wamechukua bima dhidi ya ugaidi na kampuni ya GA Insurance. 14 Riverside huwa na biashara tofauti zikiwemo ni pamoja na biashara rejareja, vyombo vya habari na biashara zingine ikiwemo hoteli ya DusitD2. Hoteli hiyo ilitarajiwa kufunguliwa mapema Juni, lakini tarehe ya kufunguliwa imesongeshwa hadi Agosti, kulingana na habari zilizoko katika tovuti yake.
Hata hivyo, hoteli hiyo bado inapokea maombi kutoka kwa wateja kuwahifadhia vyumba au kumbi.
Kundi la kigaidi la al-Shabaab lilikiri kuhusika katika shambulizi hilo, ambalo pia liliacha baadhi ya wateja wakiwa na majeraha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |