• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • VOLIBOLI: Kufuzu Voliboli ya wanawake Afrika-Kenya watumia wembe ule ule kuwanyoa Uganda

    (GMT+08:00) 2019-05-23 08:57:50
    Kenya ilitolewa kijasho na Uganda katika seti ya kwanza kabla ya kuwanyoa seti 3-0 katika mechi ya mwisho ya ukanda wa tano na kufuzu kushiriki voliboli ya wanawake kwenye mashindano ya bara Afrika (All-African Games) katika ukumbi wa Lugogo jijini Kampala.

    Malkia Strikers ilikuwa alama moja tu mbele ya Uganda 21-20 katika seti ya kwanza kabla ya kushinda wenyeji hao 25-20. Baada ya kubabaishwa katika seti ya kwanza, Kenya ilirejea katika seti mbili zilizofuata kwa nguvu zaidi na kuzinyakua 25-17, 25-16, mtawalia.

    Kenya sasa itaenda nchini Mororcco katika mashindano ya voliboli ya wanawake Afrika.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako