• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Serikali ya Yemen yasitisha mikutano na tume ya usimamizi ya UM

    (GMT+08:00) 2019-05-23 10:48:17

    Msemaji wa jeshi linalounga mkono serikali ya Yemen katika pwani ya magharibi mwa nchi hiyo Waddah Dubaish amethibitisha kuwa, wawakilishi wa serikali ya Yemen kwenye Kamati ya Uratibu wa Urejeshaji Mpya RCC katika mji wa bandari wa Hodeidah wamesitisha mikutano yao na kiongozi wa kamati hiyo, Michael Lollesgard. Amesema sababu ni kuwa kikosi cha serikali hakiruhusiwi kuingia katika bandari za Hodeidah kusimamia kujitoa kwa kundi la Houthi. Pande hasimu nchini Yemen zilifikia makubaliano chini ya Umoja wa Mataifa mwezi Disemba mwaka jana mjini Stockholm, ambayo yalihusisha kusitishwa vita mjini Hodeidah na kuanzishwa kwa kamati ya RCC ili kusimamia kuondoka kwa vikosi vya serikali na kundi la waasi katika mji huo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako