Kiongozi wa baraza la chini la Uingereza Andrea Leadsom amejiuzulu kutokana na kutoridhika zaidi na uongozi wa waziri mkuu, siku moja baada ya waziri mkuu Theresa May kupendekeza makubaliano mapya ya Brexit. Amesema haamini kuwa Uingereza itakuwa nchi yenye mamlaka halisi kwa mujibu wa makubaliano hayo, na kuongeza kuwa kura za maoni za mara ya pili zitazusha mpasuko, na hakubali serikali kujirudi nyuma.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |