Waziri wa polisi wa Afrika Kusini Bheki Cele jana amesema, maandalizi yote ya kuapishwa kwa rais Cyril Ramaphosa yamekamilika, huku usalama katika eneo ambalo hafla hiyo itafanyika Jumamosi mjini Pretoria umeimarishwa.
Bw. Cele amesema polisi zaidi 2,500 watapelekwa kuzunguka uwanja wa Loftus Versfeld ambapo hafla hiyo itafanyika. Amesema viongozi 40 wa nchi mbalimbali na watu karibu 34,000 wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |