Baada ya kuenea habari katika mitandao ya kijamii kuwa mshambuliaji wa kimataifa wa Ghana Asamoah Gyan ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Ghana kuelekea michuano ya mataifa ya Afrika AFCON 2019 itakayofanyika Misri kutokana na kuvuliwa unahodha hatimaye amebadili mawazo hayo.
Asamoah amebadili mawazo hayo baada ya rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo kumuomba afute uamuzi huo na kuamua kurejea timu ya taifa kama ilivyokuwa awali, Asamoah kwa heshima ya taifa lake na rais wa nchi yake ameamua kubadili maamuzi hayo na kuamua kurudi kulitumikia taifa hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |