Timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba kila upande ya Kenya almaarufu Shujaa, imeimarisha mazoezi yake kabla ya kuanza kampeni ya kutafuta alama kwenye michuano ya raga yatakayopigwa jijini London Uingereza kuanzia kesho Mei 25 na 26.
Shujaa inashikilia nafasi ya 13 kwa alama 26, alama nne pekee kutoka nafasi ya 15 ambayo Japan inakodolea macho kushushwa ngazi
Katika mchezo wa kesho, Kenya itavaana na Fiji, Samoa na Ufaransa kwenye mechi za kundi B.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |