Klabu ya Borrusia Dortmund imekamilisha uhamisho wa mdogo wake Eden Hazard anayeitwa Thorgan kutoka kwa wapinzani wao wa Bundesliga, Borussia Monchengladbach.
Thorgan mwenye umri wa miaka 26 amesaini kwa dau la pauni milioni 30. Akiwashukuru klabu yake ya zamani, Thorgan amesema miaka mitano aliyochezea klabu hiyo alipata mafanikio makubwa na kujifunza mengi, ameahidi kuendelea kufanya vizuri na klabu yake mpya ili wasijutie kumsajili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |