• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Utouh ataka uwazi ripoti za CAG

    (GMT+08:00) 2019-05-24 20:14:51
    Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mstaafu, Ludovick Utouh, amesema ripoti za ukaguzi zinazofanywa na Ofisi ya CAG zinapaswa kuwa taarifa za wazi kwa umma.

    CAG huyo mstaafu alitoa kauli hiyo katika mapitio ya ripoti ya CAG kwa mwaka 2017/2018 kwa wakurugenzi wa mtandao wa asasi za kiraia nchini wa kanda ya kati, katika kikao kilichofanyika jijini hapa.

    Alisema ripoti hizo zinaonyesha mapato na matumizi ya fedha za bajeti zilizopitishwa na bunge ambazo kwa kiasi kikubwa zinatokana na walipa kodi, hivyo zinatakiwa kuwa wazi.

    Utouh ambaye pia Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wajibu, alisema ripoti hizo ndilo jicho la Watanzania kwenye usimamizi wa rasilimali zao kwa kuwa ndizo pekee zinazochanganua mapato na matumizi ya bajeti na utekelezaji wake.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako