Balozi wa China nchini Marekani Bw. Cui Tiankai jana alihojiwa na kituo cha televisheni cha Marekani Bloomberg akisema kuwa, mazungumzo na mawasiliano yaliyo chini ya msingi wa usawa ndio njia pekee ya kutatua mgogoro wowote kati ya China na Marekani.
Bw. Cui Tiankai amesema, sababu ya kuwepo kwa sintofahamu kwenye mazungumzo ya uchumi na biashara kati ya China na Marekani ni kutokana na Marekani kubadilisha msimamo wake mara kwa mara. Amesisitiza kuwa msimamo wa China siku zote haubadiliki, lakini wa Marekani umekuwa ukibadilika badilika hata hivyo amesema China itaendelea kujitahidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |