Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) anayekipiga katika klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Ally Samatta, ametua jijini Dar es Salaam akiwa ametoka kuisaidia klabu yake hiyo kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya nchini humo kwa mara ya kwanza baada ya miaka nane kupita.
Wadau wa soka wameanza kuuliza endapo Samatta atarejea Ubelgiji kuichezea timu yake ya KRC Genk msimu wa 2019/2020 ama ataenda Uingereza kujaribu soka la huko ili kukamilisha ndoto yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |