Serikali ya Ethiopia imesema, Bustani ya Viwanda ya Kilinto iliyojengwa na kampuni ya China imeboresha nia ya nchi hiyo ya kuvutia kampuni za kimataifa za madawa duniani.
Tume ya Uwekezaji ya Ethiopia (EIC) imesaini makubaliano ya uwekezaji na kampuni 10 za kimataifa ambazo zimeonyesha haja kubwa ya kufungua viwanda vyao ndani ya Bustani hiyo. Pia Tume hiyo imesisitiza kuwa, bustani hiyo ya viwanda, mara itakapotumika kikamilifu, itaongeza uwezo wa nchi hiyo kuvutia kampuni zaidi za kigeni katika sekta ya madawa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |