Rais Mahmoud Abbas wa Palestina amesema "Makubaliano ya Karne" yaliyopendekezwa na Marekani na mkutano uliopangwa kufanyika Juni, 25 nchini Bahrain "ni ya kinjozi". Amesema njozi hizo hazitaweza kuwafikisha watu wa Palestina popote, na hawahitaji msaada kwani wanaweza kujenga taifa lao wenyewe. Ameongeza kuwa suala la Palestina linatakiwa kutatuliwa kwa njia ya kisiasa, na lengo lake la mwisho ni ujenzi wa taifa huru la Palestina na mji wake mkuu ukiwa Jerusalem.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |