• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Idadi ya watu waliofariki kwenye mapigano mjini Tripoli, Libya yafikia 562

    (GMT+08:00) 2019-05-28 09:11:28

    Shirika la Afya Duniani WHO limesema watu 562 wameuawa na wengine 2,855 kujeruhiwa katika mapigano ndani na karibu na mji mkuu wa Libya, Tripoli. WHO imeongeza kuwa kati ya watu waliouawa, kuna wafanyakazi wawili wa afya. Jeshi lenye makao makuu mashariki mwa nchi hiyo linaloongozwa na Khalifa Haftar limekuwa likifanya kampeni ya kijeshi tangu mapema mwezi Aprili ili kudhibiti mji wa Tripoli, ambao ni makao makuu ya serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako