• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Washirika wa UM kushirikiana na Sudan Kusini kuimarisha mfumo wa sheria kuhusu unyanyasaji wa kijinsia

    (GMT+08:00) 2019-05-28 09:19:47

    Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) linashirikiana na Sudan Kusini kuimarisha mfumo wa sheria ili kusaidia kupambana na ukatili wa kijinsia.

    Mwakilishi wa shirika hilo nchini Sudan Kusini Bi. Mary Otieno amesema, nchi hiyo inahitaji sheria ya kitaifa inayounganisha pamoja sheria zote tofauti na kanuni za adhabu zinazohusiana na unyanyasaji wa kijinsia.

    Bi. Otieno amesema, UNFPA, wizara ya ustawi wa jamii, jinsia na watoto, kwa kushirikiana na wizara ya sheria na mambo ya kikatiba wameanza mchakato wa kuunda mfumo bora wa sheria wa kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia nchini humo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako