Atalanta imefuzu kwa mara ya kwanza kucheza ligi ya mabingwa tangu klabu hiyo ianzishwe baada ya kutoka nyuma na kuichapa Sassuolo kwa mabao 3-1.
Baada ya kumaliza msimu huu kwa kishindo, ikiwemo kupata sare ugenini dhidi ya mabingwa Juventus, Atalanta imeandika rekodi kubwa msimu huu katika ligi ya Serie A.
Mabao ya Duvan Zapata, Alejandro Dario Gomez na Mario Pasalic yalitosha kuihakikishia Atalanta kupata tiketi ya kucheza ligi ya mabingwa Ulaya kutokana na uzembe wa AC Milan.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |