Lile dili la mchezaji wa Yanga Ibrahim Ajibu kwenda TP Mazembe ya DRC kufeli limetolewa ufafanuzi na uongozi wa Yanga baada ya kuleta mjadaa mzito.
Kwa mujibu wa Kaimu katibu wa klabu ya Yanga, Omar Kaya, amebainisha kwamba, TP Mazembe walikiuka taratibu na kufanya mazungumzo na mchezaji binafsi badala ya klabu.
Amesema viongozi wa Yanga wameishangaa TP Mazembe kushindwa kuonyesha weledi, na baadaye kuona taarifa mitandaoni kuwa wameshindwana na mchezaji huyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |