SOKA: Simba yawasili Morogoro kwa kishindo, tayari kukabidhiwa kombe
Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara Simba ya Dar es salaam imewasili mjini Morogoro tayari kwa mchezo wa mwisho wa ligi kuu itakapokutana na Mtibwa Sugar leo jioni kwenye uwanja wa Jamhuri na itakabidhiwa kombe.
Samba imechukua ubingwa kwa mara ya pili mfululizo na inakuwa ni mara yao ya 20 kutwaa ubingwa huo huku watani wao wa jadi Yanga wakisalia kuwa ni mabingwa wa historia kwa kutwaa taji hilo mara 27.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |