Mjumbe maalumu wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mkutano ujao wa kilele wa mabadiliko ya hali ya hewa Luis Alfonso de Alba amesema nchi mbalimbali zimeeleza kupenda kushiriki katika mkutano huo. Amesema kuna nchi 18 zinazoendesha kwa pamoja mashirikisho na pia zaidi ya nchi 40 zinashiriki kwenye mashirikisho hayo yanayopitia hatua halisi zinazoweza kuwasilishwa kwenye mkutano huo wa kilele. Ameongeza kuwa nchi hizo zimeeleza kukubali kubadili majadiliano kuwa hatua halisi za utekelezaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |