Wenyeji Kenya wamejawa na matumaini ya kufanya vyema kwenye mashindano ya voliboli ya wanaume ya ukanda wa tano Juni 2-9 mwaka huu jijini Nairobi.
akizungumza baada ya kutaja kikosi hicho, kocha Moses Epoloto amesema wanajiandaa vyema na wako tayari kwa mashindano. Mataifa mengine yatakayoshiriki mashindano hayo ni Wenyeji Kenya, Uganda, Rwanda, Misri, Tanzania, Sudan, Somalia, Ethiopia, Burundi, Sudan Kusini, Djibouti na Eritrea.
Mashindano haya yatatumiwa kuchagua timu itakayoshiriki michezo ya bara Afrika ya All-African Games itakayofanyika jijini Rabat nchini Morocco Agosti 19-31 mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |