Mmiliki wa klabu ya Newcastle United, Mike Ashley ameripotiwa kufikia makubaliano ya kuiuza timu hiyo kwa mpwa wa mmiliki wa Manchester City, Sheikh Mansour kwa dau la pauni milioni 350.
Gazeti la The Sun limeripoti kuwa, mmiliki huyo mpya anayejulikana kwa jina la Khaled bin Zayed Al Nehayan ni miongoni mwa wanafamilia ya kifalme kutoka Abu Dhabi ambapo mwaka jana alishindwa kuinunua Liverpool baada ya kutakiwa kutoa dau la pauni bilioni mbili.
Taarifa zinaeleza kuwa tayari mkataba baina ya Ashley na Khaled umeshasainiwa tayari kuichukua klabu hiyo kwa pauni milioni 350 na tayari umeshafikishwa kwa wanaohusika na ligi kuu. Mpaka sasa klabu ya Newcastle haijatoa taarifa rasmi
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |