Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), linatarajia kujenga viwanda vya kusindika mazao ya uvuvi nchini ikiwa ni moja ya mikakati yake. Hii ni kauli yake yake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdalla Ulega, ambaye pia wizara yake inaendelea kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika sekta ya uvuvi kwa kuweka mazingira mazuri, ikiwamo uwapo wa malighafi kwa viwanda vya kusindika mazao ya uvuvi. Hadi sasa kuna viwanda vitano vya kusindika mazao na uvuvi katika ukanda wa Pwani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |