Watu saba wamefariki na wengine kadhaa hawajulikani walipo mjini Budapest, Hungary baada ya boti mbili za utalii kugongana jana usiku kwenye mto Danube na kusababisha boti moja kuzama. Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Hungary, boti iliyozama ilikuwa na watu 34. Hadi sasa watu 15 wameokolewa, 7 wamethibitishwa kufa na wengine 12 hawajulikani walipo. Kazi za uokoaji bado zinaendelea na chanzo cha ajali hiyo bado hakijulikani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |