Benki ya dunia imeidhinisha mkopo wa dola milioni 750 kwa Kenya kufuatia ombi lililotolewa na serikali.
Jumatano benki hiyo imesema kuwa mkopo huo utafadhili shughuli za mageuzi muhimu, kuhimiza uwazi, ushindani na kupunguza ufisadi kwenye sekta ya kilimo.
Mkopo huo pia kwa mujibu wa benki ya dunia utasaidia uendelezaji wa mpango wa serikali wa dijitali kama vile utoaji wa vitambulizho vipya na kusaidia kufikisha huduma za intaneti kwa wakenya wote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |