Mwenyekiti wa Gor Mahia ya Kenya, Ambrose Rachier amesisitiza kuwa itawalazimu kumsaka nyota wa kigeni atakayejaza nafasi ya Jacques Tuyisenge haraka iwezekanavyo.
Hii ni licha ya Paul Were wa Harambee Stars ambaye amepania kutoongeza mkataba wake na AFC Leopards huku akihusishwa kutua Gor Mahia.
Tuyisenge mzaliwa wa Rwanda yuko mbioni kusaini mkataba wa kuichezea Petro Atletico ya Angola.
Kwa mujibu wa Rachier, uongozi wa Gor Mahia unalenga kuanzisha mazungumzo na wachezaji wawili wa kigeni kwa matarajio kwamba mmoja wao atakubali kujiunga nao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |