"Nafikiri hii ndio kwaheri kutoka kwangu lakini kwenye mpira huwezi jua" ni maneno machache ya Eden Hazard kuashiria kumaliza safari yake ndani ya klabu ya Chelsea baada ya kumalizika kwa mchezo dhidi ya Arsenal kwenye fainali ya kombe la Europa.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhamia Real Madrid na amesema kwa sasa anasubiria klabu hizo kukubaliana.
Kocha wa Chelsea Maurizio Sarri amesema anaheshimu maamuzi ya Hazard, Hazard mwenye umri wa miaka 28, alijiunga na Chelsea akitokea Lille ya Ufaransa kwa dau la pauni milioni 32.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |