Joshua amevuliwa ubingwa wa dunia wa uzito wa juu baada ya kupigwa kwa Technical Knock Out (TKO) raundi ya saba ya mchezo huo.
Ruiz hakuwahi kuangushwa kabla, lakini jana aliangushwa raundi ya tatu, kabla ya kuinuka na kuendelea na pambano. Joshua mwenye urefu wa futi sita atajaribu kurejesha mataji yake ya IBF, WBO na WBA katika pambano la marudiano mwezi Novemba mwaka huu. Hili ni pambano la kwanza Joshua kupoteza baada ya kushinda mapambano yote 22 ya awali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |