Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya reli ya TAZARA imepitisha mpango wa kusafirisha tani laki 3 za mizigo katika mwaka huu wa fedha.
Taarifa iliyotolewa na TAZARA imesema, bodi hiyo pia imepitisha mpango wa kusafirisha abiria laki 8 na kushirikisha zaidi sekta binafsi ili kukuza uchukuzi wa reli hiyo.
Taarifa pia imesema, bodi hiyo imetaka mamlaka ya TAZARA kutafuta njia inayofaa ya kuhimiza ushirikiano kati ya Sekta za umma na Sekta Binafisi katika kufadhili matumizi mapya ya vichwa vya treni visivyotumika na maeneo ya wazi yasiyotumika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |