Wilder mara kadhaa amekuwa akimtuhumu Joshua kwa kuzuia pambano lao kwa kutengeneza vikwazo lukuki ili wasikutane ulingoni.
Amesema, Joshua amekuwa akishinda mataji kwa kubebwa lakini safari hii amekutana na kisiki na ndio maana amepigwa. Promota wa Joshua Eddie Hearn ametangaza kuwa bondia wake atarejeana na Ruiz kabla ya mwaka kuisha kwenye mwezi Novemba ama Disemba jijini London.
Hearn amebainisha kwa kwa sasa mazungumzo yoyote ya kuzipiga dhidi ya Fury ama hata Wilder yamesitishwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |