Kikosi cha kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kimesema askari wake wameimarisha shughuli za kibinadamu zinazolenga kuboresha maisha ya wasomalia katika mji wa mpakani wa Dhobley na maeneo ya jirani. Ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Eid ul-fitr baada ya mfungo wa mwezi wa Ramadhani, askari hao wamegawa chakula na dawa kwa watu waliokimbia makazi yao mjini Dhobley. Pia hivi karibuni askari hao walikarabati barabara za mji huo ili kurahisisha uchukuzi wa bidhaa na huduma.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |