Rais Donald Trump wa Marekani ambaye yupo ziarani nchini Uingereza amesema, anapenda kusaini makubaliano mazuri ya biashara kati ya nchi hizo mbili baada ya Brexit. Naye waziri mkuu wa Uingereza Bi. Theresa May alipokutana na waandishi wa habari akiwa na mgeni wake huyo, amesema nchi hizo mbili zina uhusiano maalumu ya kihistoria, lakini zina maoni tofauti katika baadhi ya masuala yakiwemo mabadiliko ya hali ya hewa na suala la nyuklia la Iran.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |