Baraza Kuu la 73 la Umoja wa Mataifa limemchagua balozi wa Nigeria Bw. Tijjani Muhammad-Bande kuwa mwenyekiti wa Baraza Kuu la 74 la Umoja huo, na anatarajia kuingia ofisini rasmi mwezi Septemba mwaka huu.
Bw. Muhammad-Bande amesema, mpango wake wa kazi utazingatia zaidi kuhimiza amani na usalama, kuondoa umaskini, kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na kusukuma mbele maendeleo ya pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |