• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • IGAD yazitaka pande husika za Sudan kujizuia

    (GMT+08:00) 2019-06-06 09:21:45

    Shirika la Maendeleo la Kiserikali la Nchi za Afrika Mashariki IGAD limetoa wito kwa pande zote husika za Sudan kujizuia zaidi.

    Taarifa iliyotolewa na Shirika hilo imesema, lina wasiwasi juu ya mapigano yanayopamba moto na kuzitaka pande husika za Sudan kufanya mazungumzo kwa nia ya kufikia mwafaka.

    Shirika hilo limesisitiza haja ya kulinda amani na utulivu nchini humo na kuwataka wadau wote wa Sudan kujizuia kwa kiasi kikubwa zaidi na kupunguza hali ya wasiwasi inayozidi kuwa mbaya.

    Shirika hilo pia limerejea tena ahadi yake ya kuendelea kushughulikia hali ya Sudan kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika, ili kuisaidia nchi hiyo kukabiliana na changamoto za sasa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako